Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2018

DE GEA AWASAIDIA MANCHESTER UNITED KUTOKA SARE NA SEVILLA LIGI YA MABINGWA ULAYA UEFA

Picha
Mlindalango wa Manchester United David de Gea alifanya kazi ya ziada kuzuia makombora ya wapinzani wao Sevilla Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya mechi ya hatua ya 16 bora na kuwasaidia kutoka sare Jumatano. Kipa huyo Mhispania aliwazuia Joaquin Correa na Steven N'Zonzi kufunga kwa ustadi mkubwa, na kisha akatumia mkono mmoja muda mfupi kabla ya mapumziko kuzuia mpira wa kichwa wa Luis Muriel. United, waliokuwa wanacheza mechi yao ya kwanza ya muondoano Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya katika kipindi cha miaka minne hawakushambulia sana. Romelu Lukaku alipoteza nafasi nzuri zaidi kwao mpira wake ulipopaa juu ya lango mapema, kabla ya nguvu mpya Marcus Rashford kutupa mpira nje dakika za mwisho mwisho. Paul Pogba alianza mechi kwenye benchi, lakini akaingizwa uwanjani dakika 17 kabla ya mechi kumalizika baada ya Ander Herrera kuumia. Sevilla walimaliza mechi wakiwa wameshambulia goli mara 25 lakini mseto wa ustadi wa De Gea na makosa ya washambuliaji wao viliwazuia kuondoka na ushind...

GARBINE MUGURUZA ATINGA FAINALI DUBAI

Picha
Mchezaji Tenisi Garbine Muguruza amefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya Dubai baada ya kumshinda Caroline Garcia katika mchezo wa wa pili war obo fainali na kutinga Nusu fainali ya Dubai. Muguruza alifuzu hatua robo fainali baada ya kupata ushindi wa seti 7,5 6,2 dhidi ya mfaransa Wozniacki . Naye Bingwa wa zamani wa Gland slam kutoka Ujerumani Angelique Kerber siku ya ijumaa atacheza dhidi ya Elina Svitolina katika mchezo wa mwisho wa nusu fainali . Bingwa wa Grand Slam Muguruza amesema anamatumaini ya kufanya vizuri katika mchezo wake na baada ya kupoteza mchezo wake dhidi ya Petra Kvitova 

MITCHY BATSHUAYI APIGIWA KELELE ZA TUMBILI

Picha
Mitchy Batshuayi anasema kuwa alisikia kelele za tumbili katika eneo la mashabiki wakati ambapo Borussia Dortmund ilikuwa ikiishinda klabu ya Atalanta katika ligi ya Yuropa huko Bergamo. Mshambuliaji huyo wa Chelsea ambaye anaichezea Dortmund kwa mkopo alituma ujumbe katika mtandao wa twitter akisema: huu ni mwaka 201`8 na bado kuna kelele za sauti ya tumbili katika eneo la mashabiki....siamini. ''Natumai mulifurahia kutazama mechi za ligi ya Yuropa katika runinga'' Dortmund ilishinda 4-3 kwa jumla baada ya marcel Schmelzer kusawazisha bao lililofungwa na Wataliano hao. Mwezi uliopita , Atalanta ilipigwa marufuku ya kutocheza mechi moja baada ya beki wa Napoli kalidou Koulibaly kupigiwa kelele cha tumbili wakati wa mechi ya ligi ya Serie A.

KOREA KASKAZINI IMEZINDUA POMBE MPYA YA 'KIPEKEE'

Picha
KOREA KASKAZINI IMEZINDUA POMBE MPYA ILIYOTENGENEZWA KWA KUTUMIA MBINU MPYA NA YA 'KIPEKEE', INAARIFIWA.   KWA MUJIBU WA GAZETI LA SERIKALI  RODONG SINMUN , KIWANDA CHA KUTENGENEZA POMBE NCHINI TAEDONGGANG KINADAI KUWA MBINU YAKE MPYA YA KUTUMIA NGANO BADALA YA MPUNGA NI BORA ZAIDI KULIKO POMBE NYINGINE ZILIZOKO KWA LADHA NA HATA HARUFU NAKWAMBA IMEPOKEWA VIZURI NA WARAIBU NCHINI. TAEDONGGANG KIMEKUWA KIKITENGENEZA POMBE TANGU MWAKA 2015, NA HII HUENDA INATOKANA NA SHUTUMA KUTOKA KWA KIONGOZI MKUU NCHINI KIM JONG-UN KWAMBA POMBE INAYOINGIZWA NCHINI KUTOKA KOREA KUSINI HAINA LADHA, JARIDA LA KILA SIKU HUKO SEOUL  CHOSUN ILBO  LILIRIPOTI WAKATI HUO. KWA KAWAIDA, VYOMBO VYA HABARI KOREA KASKAZINI VINAITANGAZA POMBE HIYO KAMA UFANISI KATIKA MPANGO WA KIM JONG-UN KUINUSHA VIWANGO VYA MAISHA KATIKA NCHI HIYO YA KIKOMYUNISTI, VIKISEMA NI KUTOKANA NA ' JITIHADA ZA MUDA WOTE"KUYAFANYA MAISHA "KUWA YA RAHA ZAIDI KWA RAIA". CHOSUN ILBO ANADAI KUWA KIM...

SIRLEAF KIDEDEA TUZO YA MO IBRAHIM

Picha
RAIS WA ZAMANI WA LIBERIA ELLEN JOHNSON SIRLEAF AMESHINDA TUZO YA MWAKA YA MO IBRAHIM KWA UONGOZI WA AFRIKA - AMBAYO HUPEWA VIONGOZI WA AFRIKA AMBAO WAMEONEKANA KUWA NA UTAWALA MZURI. ELLEN JOHNSON SIRLEAF AMEKUWA MWANAMKE WA KWANZA BARANI AFRIKA KUSHIKA NAFASI YA URAIS MWAKA 2006 NA KUMALIZA MUDA WAKE MWEZI ULIOPITA BAADA YA KUHUDUMU KWA MIHULA MIWILI. KAMATI YA UTENDAJI YA TUZO YA MO IBRAHIM IMESEMA ELLEN JOHNSON SIRLEAF AMEONESHA UONGOZI WA KIPEKEE KATIKA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO ZISIZOWAHI KUTOKEA KATIKA AWAMU ZAKE MBILI ZA UONGOZI ALIPOKUWA RAIS WA LIBERIA. WAKATI ALIPOSHINDA UCHAGUZI WA RAIS NCHINI HUMO MWAKA 2005, NCHI HIYO ILIKUWA IMEGAWANYIKA KUTOKANA NA VITA VYA WENYEWE KWA WENYEWE VILIVYODUMU KWA MIAKA KADHAA NA TUZO HIYO YA AMANI ILIKUWA NI KWA AJILI YA KUMPONGEZA KUSAIDIA KUIIMARISHA NCHI HIYO. WAKOSOAJI WAKE WAMEKUWA WAKIMKOSOA KWA KUWA NA UPENDELEO, KUTOKANA NA KUWACHAGUA WATOTO WAKE KATIKA NAFASI ZA NGAZI ZA JUU NA PIA WANADAI KUWA HAKUCHUKUA HATUA ZA KUTOS...

AGONGWA NA TRENI NA KUFARIKI AKIPIGA PICHA YA 'SELFIE' THAILAND

Picha
MWANAMKE MMOJA AMEFARIKI AKIPIGA PICHA AINA YA SELFIE NA RAFIKI YAKE KATIKA BARABARA YA TRENI NCHINI THAILAND. RAFIKI  YAKE  ALISEMA KUWA WALIKUWA WAMEKUNYWA POMBE NA KUAMUA KUJIPIGA PICHA HIYO NA TRENI LAKINI HAWAKUONA TRENI NYENGINE ILIYOKUWA IKIJA KUTOKA BARABARA NYENGINE YA TRENI, KWA MUJIBU WA POLISI. MIGUU YAKE ILIKATIKA NA KUFARIKI HOSPITALINI AMBAKO ALIKUWA AMEPELEKWA KWA MATIBABU ZAIDI. RAFIKIYE WA KIUME ALIPATA MAJERAHA MABAYA. IDADI YA WATU WANAOFARIKI WAKIPIGA SELFIE KATIKA MAENEO HATARI INAONGEZEKA. KISA HICHO KILITOKEA SIKU YA ALHAMISI ASUBUHI KATIKA KITUO CHA TRENI CHA SAMSEN MJINI BANGKOK, KULINGANA NA MAAFISA WA POLISI WA WISSANUSAK SEUB AKIONGEZEA KWAMBA MAAFISA WALIKUWA WAKICHUNGUZA KILICHOTOKEA. KUCHUKUA VIDEO HUKU UMESIMAMA MBELE YA TRENI IMEONEKANA KUWA SWALA HATARI, HUSUSAN NCHINI INDIA. MNAMO MWEZI JANUARI , MTU MMOJA ALIYEKUWA AKIJICHUKUA KANDA YA VIDEO AKISUBIRI TRENI ILIOKUWA IKIKARIBIA ALIGONGWA NA TRENI HIYO MJINI HYDERABAD NCHINI ...

TOTTENHAM YAILAZA ARSENAL 1-0

Picha
MSHAMBULIAJI WA TOTTENHAM HARRY KANE NDIYE ANAYESHIKILIA HATMA YA KLABU HIYO KULINGANA NA MKUFUNZI WA KLABU HIYO MAURICIO POCHETTINO, KUFUATIA MCHEZO WAKE ULIOSAIDIA TIMU HIYO KUWALAZA MAADUI ZAO WA MJINI LONDON. KICHWA KIKALI KILICHOPIGWA NA KANE KILIMWACHA KIPA PETR CECH BILA JIBU NA KUTINGISHA WAVU KATIKA MECHI HIYO YA DEBRY YA LONDON INAYOIWEKA HOTSPURS KATIKA NAFASI YA TATU KATIKA JEDWALI LA LIGI. KANE ALIRUKA JUU YA BEKI WA ARSENAL LAURENT KOLSCIENY KATIKA DAKIKA YA 49 NA KUFUNGA KROSI ILIYOPIGWA NA BEN DAVIES . NA ULINDAJI LANGO MZURI WA CECH ULIOWEZA KUIZUIA SPURS KATIKA KIPINDI CHA PILI, AKIPANGUA MASHAMBULIO KADHAA NA HIVYOBASI KUIWEKA ARSENAL KATIKA MCHUANO HUO. MCHEZO WA TOTTENHAM ULITAWALA KILA SAFU ULIWAACHA WACHEZAJI WA ARSENAL MDOMO WAZI HUKU MCHEZAJI WA ZIADA ALEXANDRE LACAZETTE AKIKOSA NAFASI MBILI ZA WAZI, MOJAWAPO AKIWA AMESALIA NA KIPA HUGO LLORIS NA KUPIGA NJE.

MOURINHO: HATUNGEFUNGA BAO HATA KAMA TUNGECHEZA KWA SAA KUMI

Picha
MENEJA WA MANCHESTER UNITED JOSE MOURINHO AMESEMA KUWA KLABU YAKE HAINGEFUNGA BAO HATA KAMA INGECHEZA KWA SAA KUMI BAADA YA UPANDE WAKE KUPOTEZA KWA BAO 1-0 DHIDI YA NEWCASTLE. BAO LA DAKIKA YA 65 LA MATT RITCHIE LILISABABISHA THE RED DEVILS KUSHINDWA KWA MARA YA TANO MSIMU HUU. SASA MANCHESTRER UNITED WAKO NYUMA YA VIONGOZI MANCHESTER CITY KWA POINTI 16. "MIUNGU YAO YA KANDANDA ILIKUWA WAZI NAO," ALISEMA MOURINHO. "HAINGEWEZEKANA LEO." MENEJA HUYO WA ZAMANI WA CHELSEA ALISEMA KUWA NEWCASTLE WALICHEZA KAMA WANYAMA KUSHINDA NYUMBANI KWA MARA YA KWANZA TANGU OKTOBA. "HISIA ZANGU NI KUWA TUNGECHEZA KWA SAA 10 NA HATUNGEFUNGA BAO," ALISEMA. "TULIKUWA NA FURSA WAKATI TULIKUWA 0-0, ALISEMA MOURINHO, ALEXIS SANCHEZ ALIKUWA NA FURSA YA KUFUNGA NA KISHA FURSA ZINGINE DAKIKA ZA 20 NA 25 ZA MWISHO.