Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2015

KUELEKEA MAY 2,MANNY NA MAYWETHER WAONYESHA FAMILIA ZAO

Picha
MAYWEATHER NA PACQUIAO WATAMBULISHA 'USINGIZI' WAO USEMI kwamba kila mwanaume mwenye mafanikio nyuma yake kuna mwanamke, ni hivyo hivyo hata mwa mabondia wawili nyota duniani. Zimebaki wiki mbili kabla ya Floyd Mayweather na Manny Pacquiao kukutana ulingoni katika pambano la utajiri mkubwa kwenye historia ya ngumi za kulipwa. Lakini mabondia hao wawili wamehakikisha wanapata muda wa kuwa na watu hao wao wa karibuni zaidi mwishoni mwa wiki. Floyd Mayweather akiwa na mpenzi wake, Doralie Medina (kushoto) na Manny Pacquiao na mkewe Jinkee (kulia) Pacquiao akiwa na mkewe na watoto wa o(kutoka kushoto: Michael, Israel, Emmanuel, Princess na Queen Elizabeth Pacquiao aliungana na mkewe wake wa maisha yote Jinkee na watoto wao watano - Princess, Emmanuel Jnr, Israel, Queen Elizabeth na Michael. Jinkee aliwasili mjini Los Angeles mwezi uliopita, wiki tatu baada ya mumewe kuanza kambi ya maandalizi ya pambano la Mei 2 mjini humo. Wan...

MATOKEO MECHI ZOTE ZA AWALI 16 BORA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

Picha
Aprili  19  Moghreb Tétouan 1 - 0 Al Ahly Aprili  19  Raja Casablanca 2 - 2 ES Setif Aprili  19  MC El Eulma 1 - 0 Club Sportif Sfaxien Aprili  19  U.S.M Alger 2 - 1 AS Kaloum Aprili  19  AC Leopards 1 - 0 Smouha April  19  Sanga Balende 0 - 1 El Hilal Aprili  18  Al Merrikh 1 - 0 Esperance Aprili  18  Stade Malien 2 - 2 TP Mazembe

MATOKEO MECHI ZOTE ZA AWALI 16 BORA KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA MWISHONI MWA WIKI

Picha
AprilI 19 Onze Createurs 0 - 1 Asec Mimosas AprilI  19  Zamalek 0 - 0 FUS Rabat AprilI  19  C.F. Mounana 2 - 2 Orlando Pirates AprilI  18  Warri Wolves 2 - 1 FC MK AprilI  18  Royal Leopards 1 - 0 AS Vita AprilI  18  Yanga SC 1 - 1 ES Sahel AprilI  17  Amel Saad Olympic 1 - 1 Club Africain AprilI  17  Djoliba AC 1 - 2 Hearts of Oak

DEMU WA MAN CITY AMTWIKA NDOO BEKI WA ARSENAL

Picha
Kiungo wa kimataifa wa England, Jill Scott akimpiga kichwa beki wa Arsenal, Jade Bailey katika mchezo baina ya timu hizo Jumapili ya jana, kabla ya kutolewa kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja.  City ilifungwa 1-0 na mchezaji huyo aliomba msamaha baadaye leo kwa tukio hilo

NGASSA HURU YANGA,AMALIZA MKATABA WAKE

Picha
KUANZIA jana, Mrisho Khalfan Ngassa (pichani kushoto) si mchezaji wa Yanga SC, kufuatia kumalizika kwa Mkataba wake. Lakini kwa mujibu wa kanuni za soka, ataendelea kuichezea timu hiyo kumalizia msimu, kwa kuwa amesajiliwa kucheza mashindano yote ya nyumbani na ya Afrika. gift blog inafahamu jana, Aprili 20, Ngassa amemaliza Mkataba wake wa miaka miwili Yanga SC na hajasaini Mkataba mpya. “Kwa sasa sitaki kuzungumzia masuala ya Mkataba, nataka nimalize msimu kabisa ndiyo nianze mijadala ya Mkataba mpya. Mimi ni mchezaji niliyesajiliwa Yanga msimu huu. Nitamalizia msimu, baada ya hapo mengine yatafuata,”alisema Ngassa akizungumza na  gift blog jana. Kuhusu uvumi kwamba amesaini timu ya Free State Stars ya Afrika Kusini, Ngassa alisema; “Nipo kwenye mazungumzo na timu tatu, ikiwemo hiyo Free State, nyingine ya Qatar na pia nimeletewa ujumbe kwamba AS Vita (ya DRC) na Etoile nao wananifuatilia. Ndiyo maana nasema acha nimalize msimu kwanza, sina papara,”amesema. Lakini ja...

YANGA SC NA ETOILE YAINGIZA MILIONI 231, WENYEWE ‘WARUSHA’ KUTAJA MAPATO RASMI

Picha
MCHEZO wa kwanza hatua ya 16 Bora Kombe Shirikisho Afrika, baina ya wenyeji Yanga SC na Etoile du Sahel ya Tunisia umeingiza Sh. Milioni 231, gift   blog imepata hiyo. Hata hivyo, viongozi wa Yanga SC walitupiana mpira jana kuzungumzia mapato ya mechi hiyo iliyoisha kwa sare ya 1-1 Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.   Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasilano ya Yanga SC, Jerry Muro alisema apigiwe Mhasibu azungumzie mapato. Hata hivyo, Mhasibu wa Yanga SC naye akampasia mpira Ofisa Habari na Mawasiliano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto   Kutwa nzima ya leo (jana) nimekuwa nikiwafuatilia Yanga SC wanipe taarifa ya mapato ya mechi yao niitoe kwenye vyombo vya Habari, bahati mbaya sikuwapata,”alisema Baraka. Hata hivyo, taarifa za ndani ambazo gift blog imezipata ni kwamba mechi hiyo imeingiza Sh. Milioni 231, ingawa mchanganuo haukupatikana.

MANYIKA AOMBA RADHI MASHABIKI SIMBA

Picha
Peter Manyika Jr. amewaomba msamaha Simba SC kupitia akaunti yake ya Intagram REKODI YA PETER MANYIKA SIMBA SC   Simba SC 0-0 Orlando Pirates (kirafiki aliingia dk43 hakufungwa, Afrika Kusini)  Simba SC 2-4 Bidvest Witss (Kirafiki, alifungwa nne Afrika Kusini)  Simba SC 0-2 Jomo Cossmos (Kirafiki, alifungwa mbili Afrika Kusini)  Simba SC 0-0 Yanga SC (Ligi Kuu, hakufungwa) Simba SC 1-1 Prisons (Ligi Kuu, alifungwa moja) Simba SC 1-1 Mtibwa Sugar (Ligi Kuu, aliokoa penalti, akafungwa moja) Simba SC 0-0 Express (Kirafiki, hakufungwa)   Simba SC 0-1 Mtibwa Sugar (Kombe la Mapinduzi, Zanzibar alifungwa moja) Simba SC 1-0 Mafunzo (Kombe la Mapinduzi, Zanzibar hakufungwa) Simba SC 1-0 JKU ( Kombe la Mapinduzi, hakufungwa) Simba SC 4-0 Taifa Jang’ombe (Robo Fainali Kombe la Mapinduzi, hakufungwa) Simba SC 1-0  Polisi (Nusu Fainali Kombe la Mapinduzi, hakufungwa) Simba SC 0-0  Mtibwa Sugar (Alimpisha Ivo dakika ya 90, Simba ikashinda penalti 4-3 Fain...

ADE MABAO ALAANI MAUAJI SOUTH

Picha
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Toto, Emmanuel Adebayor (pichani kushoto) amelaani mashambulizi ya Xenophobic yanayoendela Afrika Kusini dhidi ya raia wa kigeni.  Mpachika mabao huyo wa zamani wa Arsenal na Real Madrid ametumia ukurasa wake wa Instagram kuzungumzia mashambulizi hayo yaliyoibuka hivi karibuni kwamba yamelichafu bara la Afrika.  "Siwazi kuamini aina hiyo ya uzalendo ambayo inaumiza mataifa mengine. Nini kimetokea Afrika Kusini inauiza na inatia machungu,"ameandika mchezaji huyo wa Tottenham Hotspur ya England.  "Mungu ametuweka pamoja kwa sababu, hakuna harakati za binadamu mwingine ni nzuri, wote kwa pamoja, hukumu na mashambulizi kama haya ni makosa. Kwa pamoja na tunatakiwa kusema kwa Xenophobia," ameongeza 'Ade Mabao'.

LIGI KUU YA AZAM UGANDA MOTO WAWAKA LEO MAHASIMU WA JINJA

Picha
LIGI Kuu ya Azam Uganda inaendelea tena leo kwa mechi kadhaa kupigwa viwanja tofauti, macho ya wengi yakielekezwa katika mchezo kati ya mahasimu wa  Jinja, Sadolin Paints na Bul FC Uwanja wa Bugembe. Timu hizo mbili zilipokutana mara ya mwisho zilitoka sare ya 1-1, Sadolin Paints wakianza kupata bao kupitia kwa Andrew Basooma na Ivan Lubaale kuisawazishia BUL F.C. Kwa sasa, Sadolin Paints inashika nafasi ya 10 kwenye msimamo wa ligi hiyo, kwa pointi zake 28 na BUL F.C ni ya tano kwa pointi zake 37. Katika mechi nyingine, Lweza F.C iaanza kupigania kuepuka kushuka daraja watakapoifuata SC Victoria University Uwanja wa Taifa wa Nelson Mandela, Namboole. Huu utakuwa mchezo wa pili kwa Victoria University ndani ya siku mbili, baada ya Jumapili kufungwa na SC Villa 2-1 katika Robo Fainali ya Kombe la Uganda. Timu zote mbili haziko salama katika hatari ya kushuka daraja kimahesabu.  SCVU ina pointi 28 na Lweza inazo 22. Katika Uwanja wa Jeshi wa Bombo, Simba, inayofundi...

UJUZI HAUZEEKI, MAGWIJI 'WAKINUKISHA' ST ETIENNE, ZIDANE AMTESA RONALDO NA WASHKAJI WAKE

Picha
Gwiji wa Brazil, Ronaldo Lima akimiliki mpira katika mchezo maalum wa 12 wa kupiga vita umasikini Uwanja wa Geoffroy-Guichard mjini Saint-Etienne jana. Mechi hiyo ilihusisha marafiki wa Ronaldo dhidi ya marafiki wa Zinadine Zidane na nyota wengine kadhaa kama Clarence Seedorf, Fabian Barthez, Gianluca Zambrotta,  Jay-Jay Okocha, David Trezeguet na Vladimir Smicer walishiriki mchezo huo. Akina Zidane walishinda 9-7.   Kiungo wa zamani wa kimataifa wa Nigeria, Jay-Jay Okocha alicheza pia   Nyota wa zamani wa Ufaransa, Zidane akifanya vitu vyake katika mchezo huo.

VAN PERSIE ACHEMKA TIMU YA WATOTO

Picha
Mfungaji wa bao la kusawazisha la U21 ya Manchester United,   Sean Goss (katikati kushoto)  katika sare ya 1-1 na U21 ya Leicester City jana Uwanja wa King Power akipongezwa na wenzake, James Wilson (kushoto) na Robin van Persie (katikati kulia). U21 ya United ilipewa tafu na kaka zao wa kikosi cha kwanza,  Robin van Persie, Adnan Januzaj, Jonny Evans, Tyler Blackett, James Wilson na Rafael. Bao la Leicester lilifungwa na mshambuliaji, Harry Panayiotou yote yakipatikana kipindi cha kwanza .

800 WAHOFIWA KUFA MAJI

Umoja wa Mataifa unasema unahofia kuwa huenda watu 800 walifariki siku ya Jumapili, pale mashua waliyokuwa wakilitumia kuvuka bahari ya Mediterenean ilipozama karibu na Libya. Shirika la Umoja wa mataifa linalowashughulikia wakimbizi UNHCR, limekuwa likizungumza na manusura baada ya kuwasili katika kisiwa cha Sicily mapema leo Jumanne. Mkuu wa sera kwenye Muungano wa Ulaya Federica Mogherini anasema kuwa pana haja ya kuwepo hatua za haraka ili kushughulikia suala kuhusu wahamiaji katika bahari ya Mediterranean, huku akizindua mikakati kumi ya mpango wa kutanzua vifo vya wahamiaji. Mogherini, anasema kuwa mipango hiyo ni hatua kubwa ya kuzuia kupotea kwa maisha ya watu. Majukumu ya muungano huo ni kuzidisha operesheni ya uokozi, pamoja na mipango mipya ya kuharibu mashua zinazotumiwa na walanguzi wa binadamu wanaowavusha watu baharini.

NAHODHA AFIKISHWA MAHAKAMANI

Picha
      Nahodha wa mashua ambayo ilizama nje ya pwani ya Libya siku ya Jumapili ambapo mamia ya wahamiaji waliangamia amefikishwa mahakamani kwa makosa ya kuua. Maafisa nchini Italia wanasema kuwa nahodha huyo raia wa Tunisia na mhudumu mwingine wa chombo hicho pia wameshtakiwa kwa kusadia uhamiaji ulio kinyume cha sheria. Wawili hao walikuwa ni miongoni mwa manusura 27 ambao waliawasili katika kisiwa cha Sicily siku ya Jumatatu. Wawili hao wanafunguliwa mashtaka wakati Muungano wa Ulaya unapotangaza mikakati ya kukabiliana na suala la uhamiaji katika bahari ya Mediterranean. Kati ya hatua zilizotangazwa ni pamoja na kuwepo shughuli za kutafuta na kuokoa mashua huka pia kukiwa na kampeni ya kuharibu mashua zinazotumiwa kusafirisha wahamiaji.

MORSI JELA MIAKA 20

Picha
           Habari za hivi punde zinasema kuwa aliyekuwa rais wa Misri Mohammed Mosri amehukumiwa kifungo cha miaka 20 gerezani kwa kuwachochoea wafuasi wa kundi la Muslim Brotherhood kuwaua waandamanaji wa upinzani alipokuwa madarakani mwaka 2012.

ROGERS NJIA PANDA LIVERPOOL

Picha
Kocha wa klabu ya Liverpool Brendan Rodgers yupo kwenye wakati mgumu baada ya kushindwa kutwaa taji lolote katika misimu mitatu ya mwanzo ya kuwanoa vijogoo hao wa Anfield. Hii ni rekodi ambayo haijawahi tokea kwa kocha yeyote tangu mwaka 1950 ndani ya kikosi hicho. ,Je ni wachezaji wasiokidhi viwango?,au ni mbinu za kocha zilizogota mwisho?hayo ni baadhi ya maswali ambayo bado hayana majibu,huku Brendan Rodgers hata kama anakula basi chakula hakishuki uzuri kwani hajui nini hatima yake kufuatia kuboronga huko.

Wanariadha 30,00 kushiriki mbio za Boston

Picha
Zaidi ya wanariadha elfu thelathini watashiriki katika mbio za mwaka huu za masafa marefu za Boston Marathon, miaka miwili baada ya mashambulio mawili ya mabomu, kutokea katika eneo la kumalizia mbio hizo. Watu watatu waliuawa kwenye shambulio hilo na wengine zaidi ya mia mbili sitini kujeruhiwa. Siku ya Jumanne, jopo maalum litaanza kuamua ikiwa mmoja wa washambuliaji hao, Dzhokhar Tsarnaev, atahukumiwa adhabu ya kifo. Wiki mbili zilizopita, alipatikana na hatia ya mashtaka kadhaa ya uhaini ikiwemo kutumia silaha za maangamizi kuua watu watatu katika mbio hizo za marathon, kuwaua afisa wa polisi siku chache baada ya shambulio hilo.  
Picha
Rwanda imeteuliwa kuwa mwenye wa fainali za kombe la mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFGA Challenge Cup, Novemba mwaka huu. Katibu mkuu wa CECAFA Nicholas Musonye amethibitisha uamuzi huo. Rwanda inatazamia kutumia fainali hiyo kujiandaa kwa michuano ya fainali za kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanashiriki ligi ya nyumbani, maarufu kama CHAN. Fainali hizo za CHAN, ndio ya pili kwa ukumbwa barani na hushirikisha wachezaji chipikizi wanaocheza ligi mbali mbali nchini mwao.

WATFORD YANUKIA EPL 2015&2016

Picha
Mshambulizi wa Nigeria Odion Ighalo, amefananisha mechi mbili za Watford zilizosalia za ligi daraha ya pili na fainali, huku klabu hiyo ikikaribia kufuzu kwa ligi kuu ya Premier nchini Uingereza. Watford inaongoza kwenye msimamo wa ligi hiyo kwa alama moja, huku ikiwa imesalia na mechi moja ya ugenini dhidi ya Brighton na nyingine dhidi ya Sheffield Wednesday katika uwanja wao wa nyumbani. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, amesema wameafikia matokeo hayo kwa sababu ya nia, ila amesisitiza kuwa ni sharti washinde mechi hizo zilizosalia. ''Tayari tunayo tikiti ya kupandishwa daraja na kamwe hatuwezi kupoteza nafasi ya kuandikisha historia'' Alisema Ighalo. Ushindi wao wa bao moja kwa bila dhidi ya Birmingham siku ya Jumamosi ilifufua matumaini ya Watford, na kuweka katika nafasi nzuri kuliko Bournemouth, ambayo inashikilia nafasi ya pili sawa na Middlesbrough lakini inadumishwa na idadi ya magoli. Msimu wa mwaka wa 2012/13, Watford ilipoteza nafa...

ASTON VILLA YAJIAMINI KUWEZA KUTWAA FA

Picha
Baada ya Aston Villa kushinda bao 2-1 dhidi ya Liverpool katika mechi ya nusu Fainali michuano ya FA Cup,sasa kocha wa Aston Villa Tim Sherwood anasema wanajinoa kuwakabili Arsenal katika mechi ya fainali. Hata hivyo amesema kuwa wanatakiwa kujiandaa vilivyo kwani Arsenal katika mechi za awali walizocheza nao waliwahi walipewa kipigo cha 3-0 na 5-0 hivyo akasema maandalizi wanayopaswa kuyafanya si ya mzaha. Sherwood amesema kuwa kuna kazi kubwa ya kufanyika ya maandalizi kuanzia sasa hadi siku ya May,30mwaka huu. Tutakachotakiwa kukifanya nikujilinda,lakini wakati huo huo kushambulia na kuhakikisha tunawashinda Arsenal kocha wa aston villa  tim sherwood kocha wa arsenal,arsene wenger

WASAUZI WATULIZWA

Picha
Mfalme wa Jamii wa Wazulu nchini Afrika Kusini, Goodwill Zwelithini, anatarajiwa kutoa wito kwa raia wa nchi hiyo kujiepusha na ghasia, kufuatia kuongezeka kwa mashambulio ya kibaguzi nchini humo. Mfalme huyo ameshutumiwa kwa kuchochea mashambulio hayo ambayo yamesababisha vifo vya watu saba. Zwelithini, alinukuliwa akisema kuwa raia wote wa kigeni wanapaswa kurejea katika mataifa yao. Zaidi ya watu mia tatu wamekamatwa kuhusiana ghasia hizo. Maelfu ya watu wanatarajiwa kufurika uwanja mmoja ulioko mji wa Mashariki wa Durban kusikiliza hotuba hiyo ya Mfalme Zwelithini. Amekariri kuwa matamshi yake hayakufahamika. Miongoni mwa washukiwa waliokamatwa hivi karibuni na wanaume watatu ambao wanatuhumiwa kuhusika na mauaji ya rais mmoja wa Mozambique katika eneo la Alexandra viungani mwa mji mkuu wa Johannesburg. Picha kadhaa zimeonyesha Emmanuel Sithole akindungwa kisu huku umati mkubwa ukitizama.   Rais wa nchi hiyo Jacob Zuma, amesema mashambulio hay...

ARSENAL IYOOOOOOOOO FAINALI FA

Picha
Reading ilikuwa ikicheza kufa na kupona ili kushiriki katika mechi ya fanaili ya kombe la FA katika uwanja wa Wemble,ambayo ni kwa mujibu wa mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger. Reading ilitoka nyuma na kusawazisha na kufanya mechi hiyo kuchezwa katika mda wa ziada. Vilvile walishindwa kutumia nafasi muhimu kuilaza Arsenal. Makosa ya kipa Adam Federic yalipaatia Arsenal ushindi huku mechi hiyo ikikamilika 2-1 kupitia mabao yaliofungwa na mchezaji nyota wa Arsenal Alexei Sa nchez

CHELSEA YAWATANDIKA MAN UTD

Picha
Mkufunzi wa kilabu ya Chelsea Jose Mourinho amesema kuwa wachezaji muhimu wa Manchester United walizuia katika mechi iliochezwa kulingana na mahitaji yake. Kocha huyo sasa anasema kuwa timu yake inaelekea kushinda ligi baada ya kuichapa Manchester United 1-0 katika uwanja wa darajani na kusonga pointi kumi mbele ya Arsenal ambao wako nafasi ya pili. United ilitawala mchezo na ilikuwa na nafasi nyingi ikilinganishwa na viongozi hao wa ligi. Mourinho:Tuliandaa mechi hiyo ichezeke ilivyokuwa.ni mechi tuliotarajia na ilichezwa kulingana na mpango wetu. Chelsea watatawazwa kuwa mabingwa iwapo watashinda dhidi ya Chelsea ama Leicester katika mechi mbili zijazo,baada ya kuishinda Manchester United ambayo iko nafasi ya tatu kupitia bao la Eden Hazard. OSCAR   AKIWA KAZINI

BALOTELL AONGOZA KWA KUBAGULIWA ZAIDI EPL 2015

Picha
Mario Balotelli ndiye mchezaji aliyebaguliwa sana katika ligi ya Uingereza ,huku mchezaji huyo akipokea zaidi ya ujumbe 8000 ,asilimia 50 zikiwa ni za kibaguzi. MARIO  SUPER BALOTELL AKIUGULIA MAUMIVU  KATIKA MOJA YA MECHI ZA TIMU YAKE YA LIVERPOOL Takwimu hizo za kushtua zimeripotiwa na Kick it Out ,ambao walibaini kwamba raia huyo wa Itali alilengwa sana katika mitandao ya Twitter huku mshambuliaji wa Arsenal Danny Welbeck akipokea ujumbe 1700 asilimia hamsini zikiwa za kibaguzi. Mshambuliaji mwenza wa Balotelli katika kilabu ya Liverpool Daniel Sturridge pia alionekana kulengwa katika mitandao ya kijamii baada ya kupokea ujumbe wa 1600 asilimia 60 ikiwa ni ujumbe wenye mwelekeo wa kijinsia. Utafiti huo pia umebaini kwamba kilabu ya Chelsea ndio kilabu iliobaguliwa zaidi kwa ujumbe 20,000 huku liverpool ikiwa ya pili na ujumbe 19,000 Arsenal ikiwa ya tatu kwa ujumbe 12,000 huku Manchester City na Manchester United zikipokea ujumbe 11,000.

WILSHERE KURUDI ARSENAL IKIWA WEMBLEY

Picha
Pavel Pogrebnyak atashiriki katika mechi ya semi fainali ya kombe la FA kati ya Reading na Arsenal baada ya kupona jeraha la mguu. Naye Nathan Ake na Kwesi Appiah hawatashiriki lakini Nathaniel Chalobah na Jamie Mackie wanaweza kucheza. Kiungo wa arsenal jack wilshere  akiwa kazini Kiungo wa kati wa Arsenal Jack Wilshere huenda akaanzishwa kwa mara ya kwanza baada ya kupona jeraha la kifundo cha mguu. Hatahivyo Mike Arteta na Alex Oxlaide Chamberlain bado wanauguza majeraha. Woljciech Szczesny ataanzishwa katika goli la Arsenal. Mlinzi wa Ufaransa Mathiew Debuchy pia huenda akaorodheshwa katika kikosi hicho,baada ya kuwa nje tangu mwezi Januari ambapo alifanyiwa upasuaji wa bega lake.

CHELSEA KUWAVAA UNITED BILA YA COSTA

Picha
Chelsea wanatumai kwamba mshambuliaji Loic Remy atacheza katika mechi dhidi ya manchester United baada ya kukosa mechi dhidi ya QPR na jeraha la mguu. Mshambuliaji  hatari wa timu ya soka ya chelsea didier Drogbaaaa akishangilia moja ya mabao yake Mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa hatocheza lakini anaweza kurudi dhidi ya Arsenal wiki ijayo. Mkufunzi wa kilabu ya manchester United Luois Van Gaal atawakosa wachezaji wake wanne akiwemo Michael carrick,Daley Blind,Phil Jones na Marcos Rojo. Jonny Evans na Chris Smalling wanahudumia marufuku huku Paddy McNair na Tyler Blackett ni wachezaji wa pekee wa safu ya ulinzi wa kiungo cha kati waliosalia.

ETOILE KUTUA TZ USIKU WA MANANE

Picha
Wapinzani wa Yanga timu ya Etoile du Sahel kutoka Tunisia wanatarajiwa kuwasili saa 9 usiku kuamkia Ijumaa kwa usafiri wa Ndege ya kukodi ya kampuni ya Nouvelair bj 4870 wakiwa na msafara wa watu 56. Makamu wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tunisia (FTF), Krifa Jalel ndiye mkuu wa msafara huo akiwa na Rais wa klabu ya Etoile du Sahel (ESS) Charefeddine Ridha, wachezaji 19, benchi la ufundi lenye watu 13, waandishi wa habari 12 na wanachama 10 Timu ya Etoile du Sahel itafikia katika hoteli ya Ledger Plaza zamani Bahari Beach eneo la Kunduchi, na Ijumaa wanatarajiwa kufanya mazoezi katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. Waamuzi wa mchezo huo ni Samwel Chirindiza, Arsenio Marenguka, Celio de Jesus Musabe, Jose Maria Bachide wote kutoka nchini Msumbiji na walitarajiwa kuwasili mchana wa Alhamisi, huku kamisaa wa mchezo huo Salah Ahmed Mohamed kutokea nchini Sudan akitarajiwa kuwasili leo jioni na wote watafikia katika hoteli ya Protea iliyopo Oysterbay.