YANGA SC NA ETOILE YAINGIZA MILIONI 231, WENYEWE ‘WARUSHA’ KUTAJA MAPATO RASMI

MCHEZO wa kwanza hatua ya 16 Bora Kombe Shirikisho Afrika, baina ya wenyeji Yanga SC na Etoile du Sahel ya Tunisia umeingiza Sh. Milioni 231, gift   blog imepata hiyo.
Hata hivyo, viongozi wa Yanga SC walitupiana mpira jana kuzungumzia mapato ya mechi hiyo iliyoisha kwa sare ya 1-1 Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.  
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasilano ya Yanga SC, Jerry Muro alisema apigiwe Mhasibu azungumzie mapato.
Hata hivyo, Mhasibu wa Yanga SC naye akampasia mpira Ofisa Habari na Mawasiliano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto
 Kutwa nzima ya leo (jana) nimekuwa nikiwafuatilia Yanga SC wanipe taarifa ya mapato ya mechi yao niitoe kwenye vyombo vya Habari, bahati mbaya sikuwapata,”alisema Baraka.
Hata hivyo, taarifa za ndani ambazo gift blog imezipata ni kwamba mechi hiyo imeingiza Sh. Milioni 231, ingawa mchanganuo haukupatikana.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CHELSEA KUWAVAA UNITED BILA YA COSTA

ROGERS NJIA PANDA LIVERPOOL